Habari

Mkuu wa wilaya Hai Ole Sabaya, ameamuru kukamatwa viongozi hawa watatu, mmoja wa CCM kwa kosa hili – Video

Mkuu wa wilaya Hai Ole Sabaya, ameamuru kukamatwa viongozi hawa watatu, mmoja wa CCM - Video

Mkuu wa Wilaya ya Hai @lengai_ole_sabaya ameamuru kukamatwa kwa Viongozi watatu wa chama Cha kuweka na kukopa cha Nshala.

@lengai_ole_sabaya amewakabidhi Takukuru viongozi hao watatu wa chama hicho akiwemo aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Hai Ambae ndie Mwenyekiti wa Bodi ya Sacco’s hiyo Kutokana na Ubadhirifu wa zaidi ya Milioni 600 uliokithiri ndani ya Sacco’s hiyo .

Mkuu huyo wa Wilaya @lengai_ole_sabaya amesema Rais Magufuli amekerwa na Kuumizwa Sana kwa uwepo wa vitendo vya namna hiyo Maana vinasababisha vilio kwa wananchi.

Pia ameagiza Kukamatwa kwa watu wote walikopa na kutapeli Fedha za chama hicho Kisha kutokomea kusikojulikana

Huu ni mwendelezo wa ziara za kurejesha fedha zilizotapeliwa ndani ya vyama vya Ushirika katika Wilaya hiyo na hii ni baada ya tangazo la Siku Kumi na Nne Alilolitoa kwa Watu hao kulipa Fedha hizo kuisha tarehe ya jana.
Madeni hayo ni tangu mwaka 2005.

https://www.instagram.com/p/B58WAgGBCwt/

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents