Burudani
Picha: Rapper Gucci Mane auaga ukapera
Rapper kutoka Marekani Guccie Mane ameachana na maisha ya kisela kwa kufunga ndoa na mpenzi wake, Keyshia Ka’oir siku ya jana 10/17/ 2017.
Guccie Mane ambaye jina lake halisi ni Radric Delantic Davis, amefunga ndoa hiyo katika mji wa Miami, maeneo ya Four Seasons.
Harusi hiyo iliudhuliwa na mastaa kadha wakiwemo Diddy ‘Combs’, Kim Zolciak-Biermann, Karrueche Tran, Lil Yachty, 2 Chainz, Rick Ross, Big Sean na Jhene Aiko.
Hizi ni picha za harusi hiyo: