Burudani

Picha ya utupu yavuja mtandaoni, ni Young Dee na Amber Lulu

Dakika chache zilizopita picha ya rapper Young Dee akiwa na Amber Lulu imesambaa katika mitandao ya kijamii na kupelekea kuibua sitofahamu.

Hits maker huyo wa Bongo Bahati Mbaya ameamua kutolea ufafanuzi picha hiyo na kueleza kuwa imevuja kimakosa na alikuwa na lengo ya ku-promote vazi aina ya Scortish.

‘Nasikitishwa kwa picha inayosambaa mitandaoni.. imevuja bila ridhaa yangu ni picha iliyokua imepigwa behind the scene lengo haswa la photoshoot ni aina hii mpya ya mavazi ya aina ya ki”Scortish” kama sketi. Naomba radhi sana kwa hili! Na kwa mashabiki wote!,” ameandika Young Dee katika Instagram yake.

Young Dee na Amber Lulu wamekuwa wakidaiwa kuwa wapenzi na picha hiyo ilivyotoka ikanakiliwa kwa baadhi ya mitandao kuwa ni ujio wa ngoma yao mpya. Kwa sasa Amber lulu na hit na ngoma yake ya ‘Only You’.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents