Burudani

R. Kelly afunguka mazito, aeleza sababu za kugoma kuhudumia watoto wake

Ikiwa zimepita siku chache tangu gwiji wa muziki wa RnB duniani, R. Kelly kuachiwa huru na mahakama baada ya kufanikiwa kulipa kiasi cha dola $161k alichokuwa anadaiwa na aliyekuwa mke wake, Drea Kelly kwa ajili ya kuhudumia watoto wake, hatimaye R. Kelly amefunguka sababu za yeye kusimamisha kuhudumia watoto wake tangu mwaka 2017.

Image result for r kelly and drea kelly
Drea na R. Kelly

Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, R. Kelly amesema kuwa aliacha kutuma fedha ya kuhudumia watoto wake (3) baada ya mwanamke huyo kubadilisha namba ya simu na kuwakataza watoto wake wasimjulie hali.

Mkongwe huyo wa muziki wa kubembeleza amedai kuwa Ex wake aliwalisha sumu watoto juu yake, jambo lililowafanya waanze kumchukia.

Imeelezwa kuwa R. Kelly kwa mwezi alitakiwa kulipa kiasi cha dola $20k kwa watoto wake watatu lakini hakufanya hivyo tangu mwaka 2017.

Jumamosi iliyopita R. Kelly aliachiwa huru baada ya mtu asiyejulikana kumlipia dola $161k sawa na Tsh milioni 377.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents