Habari

Rais Magufuli amerudisha heshima ya taifa letu – Humphrey Polepole

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole ameshangazwa na raia wa Namibia kwa kumtaja Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John P Magufuli  kila sehemu nchini humo huku akisema kuwa ni sifa kwa taifa letu.

Humphrey Polepole

Polepole ambaye yupo nchini Namibia kikazi kwa mujibu wa maelezo yake amesema kila mtu anayekutana nae nchini humo anamuulizia Rais Magufuli.

“Niko Namibia kwa kazi ya CCM na kila mtu anamuulizia Magufuli, Magufuli, Magufuli. Huyu Magufuli amerudisha maradufu heshima ya Taifa letu”,ameandika Polepole kwenye ukurasa wake wa Twitter.

https://twitter.com/hpolepole/status/904659876181401602

SOMA ZAIDI – Polepole ajibu baada ya kuambiwa viatu vya Nape vinampwaya

Humphrey Polepole ni moja ya viongozi wa CCM ambao wanasiasa wengi wanadai kuwa nafasi aliyopewa kwenye chama hicho ni kubwa kulinganisha na uwezo wake akiwemo  Mbunge wa Iringa mjini, Mchungaji Peter Msigwa.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents