Sanamu ya Mwl. Nyerere aliyokabidhiwa Rais Magufuli na Waziri Kigwangalla yazua gumzo mtandaoni, Wengine waifananisha na Steve Nyerere
Jana Julai 9, 2019 kulikuwa na hafla ya uzinduzi wa Hifadhi mpya ya wanyamapori ya Burigi-Chato, Hafla ambayo ilihudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
Kwenye uzinduzi huo, Rais Magufuli alikabidhiwa sanamu ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla yenye ujumbe maalum kuhusu umuhimu wa utunzaji wa mazingira ya wanyama pori.
Muonekano wa sanamu hiyo, umezua mijadala tofauti tofauti kwenye mitandao ya kijamii wengi wakionekana kushangazwa na muonekano wake wakidai kuwa hauendani hata kidogo na sura ya Mwalimu Nyerere.
MAONI YA WADAU KUTOKA TWITTER.
Inasemekana eti… TIVU AKE ππππππ pic.twitter.com/BOpLxgNUaO
— Webiro Wakazi Wassira #TheLeader (@Wakazi) July 10, 2019
https://twitter.com/enockdotto/status/1148755906076827650
https://twitter.com/Apollomargwe/status/1148832242870968320
So ile sanamu ni ya Steve Nyerere? Sio Kambarage Nyerere tena? Au sijaelewa hizi picha wanazoziunganisha?
— Makinikia (@AskofuTZA) July 10, 2019
Huyo jamaa wasingesema ni sanamu ya Nyerere mimi kwa kweli ningejua ndie huyo BURIGI mwenyewe… @HKigwangalla lakini unatuonaje wananzengo wenzako braza ukiwa nje ya box huko?? https://t.co/7dJzrLTwP3 pic.twitter.com/9f9nxc4FR2
— Martin Maranja Masese (@IAMartin_) July 10, 2019
Wadau mbalimbali katika mitandao ya kijamii walalamikia sanamu hili wakisema halifanani na sura ya Mwalimu Nyerere huku wakilinganisha na masanamu mengine ya Nyerere Mh.. @HKigwangalla Lifanyie kazi hili lisipite hivi hivi pic.twitter.com/yYLMwqMXt9
— Herbalist (@oreganosis) July 10, 2019
Hapana! Hii si sanamu ya Mwl JK Nyerere. Walioichonga na walioipokea wana Nyerere wao vichwani, si yule tumjuaye Baba wa Taifa. Warudi kiwandani! pic.twitter.com/P05GlTt99i
— SK Media EA (@ngurumo) July 10, 2019
Japo siamini katika Masanamu LAKINI Hiyo sanamu yenu ya jana sio MWL NYERERE.
— Angry Citizen (@HamadHamis) July 10, 2019
Jamani jamani HK akimaliza misele yake utuletee majibu hapa kuhusu hii sanamu ni ya nani haswa. Maana Mwl. Nyerere β Steve Nyerere β Dr. Shika βπππ pic.twitter.com/8yuT8e107r
— BureBabaliaπ (@bure_babalia) July 10, 2019
Sanamu ya Mwl Nyerere, huyu huyu nae mjua mimi au kuna mwingine. #SioMwalimu pic.twitter.com/ciNnPHwXcf
— Cabo Luca Kangoye (@Born4mi) July 10, 2019
Huyu katika sanamu ni Nyerere au @HKigwangalla inakuwa ngumu kidogo kumuelewesha hata mtoto wa darasa la Tano pale #simamanishukeprimary maana sanamu ya Mwalimu wanaifahamu vizuri. @Msessan @Benjaminmunyoda @seif_tanzania pic.twitter.com/P2hm6yohK6
— Ntele Bh (@ntele_bh) July 10, 2019
https://twitter.com/SheriiiMalia/status/1148864636076400641
KUTOKA INSTAGRAM
dennis_louis_
mbona hii sanamu inafanana na Mzee malekela baba yake lemutuz?
seviour_son
Jamaaaaan amkeeeen Kuna Nyerere Mpya Huku πππππ…
Huyu Ndugu Yake labdaπ
mwanakhamis_masoud
Hy ni sanamu ya nani?????
itambikojunior
Ila huyo itakuwa mwalimu wa maarifa ila siyo sanamu ya mwalimu Nyerere
k_wa_tatu
@hamisi_kigwangallaΒ mkuu,
Huyo sio nyerere tunayemfahamu….
Ni vyema ukaibadili
iamkenny255
Mmmh! Huyo mbona kama Steve nyerere au macho yenu yanaona kama Mimi?
jm.shenyagwa
Naomba tuelewane, Hii ni sura ya baba wa Taifa kwa sasa hivi, siyo ya kipindi cha uhai wake. Mwisho wa mjadalaπ₯π₯π
Je, unadhani kweli sanamu hiyo imekosewa au ni macho ya watu hao wameshindwa utambuzi wa sura ya baba wa Taifa?