Habari
Serikali yatoa pole kwa familia ya Agness Masogange (+video)
Serikali ya mkoa wa Mbeya ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo, Amos Makalla imetoa pole kwa familia ya Agness Masogange kwa kumpoteza binti yao kipenzi ambaye alikuwa ni nguvu kazi kwa taifa.
RC Makalla ametoa kauli hiyo leo Aprili 23, 2018 katika kijiji cha Utengule, Mbarali mkoani Mbeya wakati akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye mazishi ya Masogange.