Habari

Soudy Brown na Maua Sama waachiwa kwa dhamana na jeshi la polisi

Mtangazaji wa kipindi cha Shilawadu cha Clouds TV na Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Maua Sama leo jioni ya Septemba 25, 2018 wameachiwa kwa dhamana ya jeshi la polisi.

Maua Sama na Soudy Brown

Soudy Brown, Maua Sama na Meneja wake Fadhili Kondo wote wanatakiwa kesho kuripoti kituo cha kati (Central Police Station) saa 4 asubuhi.

Watatu hao jana walirudishwa mahabusu baada ya kupata dhamana ya kesi ya kwanza ya kuweka maudhui mitandao bila kibali kutoka kwa mamlaka husika, lakini waliendelea kushikiliwa na jeshi la polisi kwa kile kilichodaiwa kuwa bado wanakosa lingine la kujibu, huku Mawakili wao wakizungumzia tukio la kukanyaga fedha ya Tanzania.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents