Habari
Tanzania yakabidhiwa rasmi Uenyekiti wa SADC (+Video)
Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), aliyemaliza muda wake, Bi. Netumbo Nandi Ndaitwah kutoka Namibia, amekabidhi rasmi madaraka hayo kwa Mwenyekiti mpya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi katika mkutano uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam leo Jumanne Agosti 13, 2019 .