Burudani
Vera Sidika anafuata nyayo za Alikiba
Mwanamitandao na video vixer kutoka nchini Kenya, Vera Sidika ameamua kufuata nyayo za msanii wa muziki kutoka Tanzania Alikiba kwa kuto kuwa na mtu yoyote anayemfuatilia kwenye mtandao wa kijamii.
Ukitazama akaunti ya Instagram ya mrembo huyo ambayo ni mpya ina watu 16k wanomfuatilia, Vera ameamua kufuta watu wote aliokuwa nao upande wa following siku chache zilizopita.
Akaunti ya mtandao wa Instagram wa hasimu wake, Huddah Monroe ilikuwa verified na huwenda naye mrembo huyo anapigania kupata nafasi kama hiyo baada ya kudukuliwa akaunti yake ya mwanzo.