Burudani

Video: Chemical ni mtoto wa kike kama sijapiga pia sio mbaya – Msami

Wiki chache zilizopita zlisambaa picha zikimuonyesha msanii wa muziki na dansa Msami Baby akiwa na rapper wa kike Chemical, ufukweni huku comment na chating zao katika mtandao wa kijamii wa instagram zikatafsiriwa kuwa wawili hawa wapo kwenye mahusiano ya kimapenzi.

Akiongea na Bongo5, Msamii amenyoosha maelezo na kudaikuwa kuwa kuhusu yeye na Chemical ni issue nyeti kidogo hivyo mashabiki zake wadeal na muziki wake na sio masuala ya kimapenzi kutaka kujua anatoka na nani ana nini.

“Issue ya kupiga au kupita ni issue personal kati ya mimi na Chemical kama nimepiga it’s okay coz Chemical ni mtoto wa kike na kama sijapiga pia sio mbaya,” amesema msanii huyo na bamba na ngoma ya Mdundo.

“Kitu ambacho mashabiki zangu wanatakiwa ku-deal nacho ni muziki wangu mambo haya sijui nimepiga nani nini na nini sio kazi yao, kazi yao wao ni kuangalia mimi naleta nini kwenye muziki nafanya nini kwenye muziki ishu za mapenzi  haitakiwa kuwa sehemu talent yangu. Mimi nimeingia kwenye muziki kwa sababu nataka watu waelewe, waone uwezo wangu wa kucheza na ku-perfoms at the same time nikiwa naimba yani isiwe waone nachapa nani napiga nani sio shughuli ambayo imenileta kwenye muziki,” ameongeza Msami.

Wawili hao wameshawahi kufanya ngoma moja iitwayo ‘So Fine’ na picha waliokuwa wakiziweka katika mtandaoni zilikuwa sehemu ya video kutoka kwenye ngoma hiyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents