Wafanyabiashara wacharuka “Wasanii wanatuharibia watoto wetu, Diamond anatuangusha bora Alikiba” – Video
Wafanyabiashara wacharuka "Wasanii wanatuharibia watoto wetu, Diamond anatuangusha bora Alikiba" - Video
Baadhi ya Wafanyabiashara katika soko la Kariakoo wametoa ya moyoni kuhusu wasanii wanatumia mitandao ya kijamii kupost vitu visivyokubalika katika jamii
Baadhi yao wamesema kuwa watoto wao wanaongoza kuwafautilia sana kwenye mitandao ya kijamii lakini pia wakiwa kama vioo vya jamii wanapaswa kufanya vitu ambavyo jamii itaiga hata watoto watajifunza mengi kutoka kwao.
Mmoja wa wafanyabiashara hao amesema kwamba kuna baadhi ya wasanii wamemvunja moyo maana alikuwa anawapenda sana akiwatolea mfano kama Meninatz Diamondplatnumz Harmonize na wengine lakini akiongeza kuwa angalau msanii anayejitahidi ni Alikiba “Watoto wangu wanampenda sana Alikiba na kwa sasa wameshina suruali zinaitwa #Kibastyle wanazipenda kweli yani, Dudu baya naomba abadilike “
By Ally Juma,