Habari

Wasanii wakubwa wa Gospel nchini Kenya, wakiri kumuingilia kimwili mwanamke ‘Threesome’ na kumuambukiza gonjwa la zinaa

Wasanii wakubwa wa muziki wa Injili nchini Kenya, DK Kwenye Beat na Hope Kid wamejikuta katika kipindi kigumu nchini humo baada ya kukiri kumuingilia kimwili mwanamke aliyelalamika kwenye vyombo vya habari kuwa ameambukizwa gonjwa la zinaa (STI).



, Hopekid na DK Kwenye Beat

DK kwenye Beat yeye ndiye aliyeanza kukiri kushiriki tukio hilo, ambapo amejirekodi video ya dakika 5, huku akihojiwa na muimbaji mwingine wa Gospel, Size 8.

https://www.instagram.com/p/BtTsxXFFboT/

DK Kwenye Beat amemuomba msamaha mchumba wake, Sherry Shanice na mashabiki wake kwa kitendo hicho.

Imeelezwa kuwa msichana huyo anatoka Mjini Nakuru, na alianza mawasiliano kwa njia ya mtandao na masanii Hope Kid.

Msichana huyo (20) ambaye ameambukizwa gonjwa la ngono, amesema alitongozwa na Hope Kid na kisha baadae kumtumia nauli ya kwenda Nairobi kuonana.

Anasema alipofika Nairobi mwezi Novemba mwaka jana , Hope Kid alimpeleka nyumbani kwa DK Kwenye Beat ambapo walimfanyia unyama huo kwa wiki moja.

Katika maelezo ya msichana huyo, amedai kuwa baada ya kufanyiwa kitendo hicho mwezi mmoja baadae DK kwenye Beat alimfuata tena Binti huyo huko Nakuru ambapo anadai alifanya naye mapenzi bila jambo lililopelekea kuambukizwa gonjwa hilo la zinaa Human Papilloma Virus (HPV) .

Kwa upande mwingine, Hope Kid naye amewaomba radhi mashabiki wake na kudai kuwa alianguka kiimani.

I write this with a very heavy heart. I have done wrong before God and man. I am truly sorry. I am not a righteous man. I am a young man who has made mistake (which I am sorry for). I sincerely apologize to all who have been hurt as a result of my action.

I believe that if we confess our sins, God is faithful and just to forgive us of all our sins and cleanse us from all unrighteousness. I have repented of my sins and I am pursuing a life that is pleasing to Christ to the best of my ability. I have some pastors and some godly men who are walking with me in this path and I thank them for standing with me in this difficult time.

To all my fans, supporters, family and friends: I apologize for letting you down. I have fallen but God will raise me up. God will work this around for his glory!

I urge you all to pray for me as I go through this restoration process. God bless you!

Hata hivyo, licha ya kuomba msamaha Wakenya wengi wameendelea kuwaandama wasanii hao kwa kutaka wachukuliwe hatua za kisheria. Tazama video

https://youtu.be/3ASq7F6-nWc

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents