Burudani

Wasanii watatu wa Nigeria Singah, Joeboy na Wurld kutua Tanzania kupiga show ya pamoja (+Video)

Wasanii watatu kutoka nchini Nigeria wanatarajiwa kutua nchini Tanzania kwa ajili ya kutoa show ambayo inatarajiwa kuwa ya kipekee kutokana na aina ya wasanii wanaotarajiwa kutua.

Wakiongea na waandishi wa habari wahusika wa kampuni ya STR8UP Vibes ambayo ni waandaaji wa show hiyo wameeleza dhumuni la kuwaleta wasanii hao Tanzania.

Wasanii hao kila mmoja ana ngoma yake ambayo imefanya vizuri sana nje ya Nigeria hususani Tanzania mfano Singahj ambaye amewahi kufanya ngoma na Nedy music kutoka Tanzania alitamba na ngoma yake ya #Teyamo huku Joeboy akitamba na #Baby na Wurld akitamba na ngoma yake ya #Mad.

Wasanii wanatarajiwa kutoa Bonge la Show mnamo tarehe 26/9/2020 jijini Dar Es Salaam.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents