Habari

Watu 5 Wafariki Dunia baada ya Jengo kuporomoka, 50 wajeruhiwa

Watu watano sasa wamethibitishwa kufariki na zaidi ya 20 wanapokea matibabu katika hospitali za karibu, huku kumi wakiwa katika hali mbaya.

Chanzo cha habari kinasema waokoaji wamewasiliana na baadhi waliofukiwa chini ya vifusi.

Awali, watu 24 waliondolewa kutoka kwenye vifusi na wengine kulazwa hospitalini kufuatia kuporomoka kwa jengo katika mji wa George nchini Afrika Kusini siku ya Jumatatu.

Wengine zaidi ya 50 bado wamenaswa chini ya vifusi vya eneo la ujenzi.

Vikundi vya utafutaji na uokoaji vilifanya kazi usiku kucha ili kuwatafuta wafanyakazi kadhaa wa ujenzi waliokuwa wamekwama kwenye jengo hilo.

Zaidi ya wafanyakazi 100 wa dharura na mbwa wa kunusa kwa sasa wako katika eneo la tukio wakitafuta manusura chini ya vifusi na kwenye matofali ya zege na kiunzi kilichochongwa.

Wanafamilia walipiga kambi katika jengo la manispaa iliyo karibu ili kusubiri habari za jamaa zao.

Mamlaka ya eneo hilo ilisema wafanyikazi 75 wa ujenzi walikuwa kwenye eneo la tukio wakati jengo la ghorofa tano lilipoporomoka.

Sababu ya kuanguka kwa jengo hilo bado haijajulikana.

Imeandikwa na Mbanga B.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents