Habari
Watumiaji wa iPhones wanaopenda kusikiliza muziki kwenye simu wapatwa na pigo
Kampuni ya Apple ipo mbioni kufuta programu wezeshi ya iTunes ya kusikiliza nyimbo kwenye simu za iPhones.
Tetesi zilizopo ni kwamba Apple wamefikia hatua hiyo, kwa sababu za kibiashara na wapo njiani kutengeneza App nyingine itakayotumika kama mbadala.
Kwa mujibu wa mtandao wa Mac Rumours umeeleza kuwa vipindi vya runinga na filamu zote zitapatikana kwenye Apple Tv Plus.
Tayari kwenye kurasa za mitandao ya kijamii ya iTunes posts zote za awali zimefutwa na hakuna maelezo yaliyotolewa.
https://www.instagram.com/itunes/