Waziri Hamisi Kigwangalla awatolea uvivu Watanzania “Ama kweli wabongo huwa hatujui tunachotaka”
Waziri Hamisi Kigwangalla awatolea uvivu Watanzania "Ama kweli wabongo huwa hatujui tunachotaka"
Kufuatila Kautli kauli aliyoitoa siku jana kuhusu nchi ya Rwanda kuingia mkataba na klabu ya PSG kutoka Ufaransa kwa ajili ya kutangaza vivutio vilivyopo nchini Rwanda kitu kilichopelekea Watanzania kuanza kuitupia lawama Wizara husika hapa nchini, Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt.
Hamisi Kigwangalla aliamua kutoa taarifa fupi kuhusu kiachoendelea kati ya wizara yenye dhamana na baadhi ya timu kutoka nje ya nchi ambazo tayari zimetuma maombi ya kuingia mkataba na Tanzania kwa ajili ya kuutangaza utalii wetu na haya ndio yalikuwa maneno ya Waziri Kigwangalla:-
“Nimekuwa nikipokea malalamiko na ushauri mwingi kufuatia ndugu zetu wa Rwanda kusaini dili naΒ @PSG_English. Tunafahamu nguvu na nafasi ya soka ya ulaya kwenye kutangaza brands. Tanzania tumefuatwa na vilabu kadhaa, bado tunachambua kabla Serikali haijaamua kama tuingie ama la.Β #TanzaniaUnforgettable,β
Baada ya Watanzania kuanza kulalamika na kusema Wizara inaiga mambo kutoka Rwanda Waziri mwenye dhamana aliamua kuutumia ukurasa wake wa Twitter na kuandika haya.
TWEET1: Ama kweli wabongo huwa hatujui tunachotaka. Ni kazi sana ku-respond kwenye matakwa yetu sisi watanzania. Wengine walianza kurusha mawe kwa serikali kuwa hatutumii fursa za uwepo wa wasanii, tulipowatumia, wakalalamika, na wengine wakasema tunakula Hata tu! π. Inaendelea.
— Dr. Hamisi Kigwangalla (@HKigwangalla) December 6, 2019
TWEET2: wengine wakalalamika kuwa Rwanda inatupita sababu wanatumia soka kujitangaza, tukarespond, kufanya utafiti na uchambuzi wa kina wa njia hii ya kujitangaza kama inalipa ama la, na kama tuingie ama la. Majuzi hapa Rwanda kaongeza mkataba mwingine tena, mkatushambulia…
— Dr. Hamisi Kigwangalla (@HKigwangalla) December 6, 2019
TWEET3: mkatushambulia kuwa tumelala, tuna vivutio vingi, iweje Rwanda atupite kujitangaza? Rwanda wako strategic zaidi yetu! Nikaona niwaeleze tu kuwa na sisi hatujakaa kimya, kuna proposal nyingi tumeletewa, kama serikali tuna utaratibu rigorous wa kufanya uamuzi, tunachambua..
— Dr. Hamisi Kigwangalla (@HKigwangalla) December 6, 2019
TWEET4: nikasema tunashughulikia taarifa tulizonazo, tukiona kuna faida kwetu kuwekeza pesa ya serikali, tutaingia huko, kama hakuna hatutoingia. Nayo imekuwa tena mbaya, tusiige Rwanda, Kwa nini tusubiri mpaka clubs zitufuate? N. K. La wema lipi ndugu zangu? ππΎπ
— Dr. Hamisi Kigwangalla (@HKigwangalla) December 6, 2019
By Ally Juma.