Burudani
Ice Boy kutoka ‘High Table Sound’ ya Barnaba azungumzia mipango ya muziki wake
Msanii wa muziki kutoka label ya ‘High Table Sound’ ya Barnaba, ‘Ice Boy’ amefunguka na kuzungumzia maisha yake ya muziki pamoja na mipango yake akiwa ndani ya label hiyo.
Akizungumza na Bongo5, Ice Boy amesema anaamini ‘High Table Sound’ inaweza kubadili maisha yake ya muziki.
“Kwa sasa nipo kwa Barnaba, tayari nimeona wapi natakiwa kwenda na kwa njia gani,” alisema Ice Boy. Kwa hiyo naweza sema hapa kwangu ni sehemu sahihi kwangu, tayari kuna kolabo za kimataifa nimefanya, kwa hiyo mashabiki wakae mkao wa kula kuna mambo mengi mazuri yanakuja,” alisema Ice Boy.