Burudani

Afande Sele atoa ujumbe kwa wazazi

Tangu mfalme wa rhymes Afande Sele atangaze kuwania ubunge mwaka 2015, amekuwa akiitumia sana Facebook kutoa ujumbe maridhawa wa mabadiliko.

Alhamis hii rapper huyo ambaye jina lake halisi ni Seleman Msindi amewashauri wazazi kuwajengea watoto wao msingi wa mapema kuhusu chanzo cha umaskini nchini.

“Tujenge misingi mpaka kwa watoto wetu kuwa umasikini tulionao, unaletwa na wachache!! Na hatutaki wala hatupendi kuona wao wakiwa na maisha mabovu, ndio maana namuonyesha njia sahihi, ili wakati wake ukifika asihadaike”, ameandika Afande.

Katika ujumbe huo Afande pia amesema, “kuna wakati maamuzi madogo sana yanaweza badilisha maisha yetu daima!! Hakuna ubaya kuhitaji mabadiliko, kama yatakua katika njia sahihi.”

Ni mrefu tangu msanii huyo mkongwe aliyetamba na ngoma kama ‘Darubini’ na ‘Mtazamo’ hajahit kwenye radio jambo ambalo limemfanya avitupie lawama baadhi ya vyombo vya habari kuwa vinauua muziki wa Tanzania kwa kupendelea wasanii wachache.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents