Habari
AFCON 2013 Finals: TB Joshua atabiri ushindi wa Nigeria kesho
Mchungaji maarufu wa nchini Nigeria Temitope Balogun Joshua amesema timu ya taifa ya Nigeria, Super Eagles kesho itaishinda Burkina Faso kwenye fainali ya kombe la mataifa ya Afrika nchini Afrika Kusini.
“Jumapili wapinzani wetu watacheza kwa kujihami sababu watakuwa wanatafuta upigaji wa penati mwisho wa mchezo. Ninachoona sitaki kukisema sababu kitawaogopesha lakini nawahakikishia kuwa tutavuka changamoto hiyo Jumapili.”
Nabii huyo amewaonya Eagles wasiwaruhusu Burkina Faso wafunge goli kwanza kwa kusema, “kama ikitokea hivyo waburkinabe watarudi nyuma kulinda goli kitu ambacho kitakuwa hatari kwa timu yetu.”