Alikiba ampa shavu Mpoki
![](https://bongo5.com/wp-content/uploads/2018/05/page-15.jpg)
Katika kuelekea mchezo maalumu wa hisani ya kuchangia elimu, msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Alikiba ametangaza kikosi cha wachezaji watakao kuwa upande wake kupambana dhidi ya kikosi cha wachezaji watakaokuwa upande wa mshambuliaji wa timu ya Taifa na klabu ya KRC Genk, Mbwana Samatta.
![Picha inayohusiana](https://bongo5.com/wp-content/uploads/2018/05/alikiba.jpg)
Kwenye kikosi hicho, Alikiba amemchukua mshambuliaji hatari wa klabu ya Simba, Emmanuel Okwi na wachezaji wengine kama John Bocco, Msuva, Erasto Nyoni, Abdu Kiba na wengineo kama inavyoonesha hapa chini kwenye picha.
Kikubwa zaidi ni kwamba Alikiba amemchagua mchekeshaji maarufu nchini Tanania, Mpoki kuwa msemaji wa timu yake aliyoichagua.
Soma kikosi cha Samatta – Samatta aweka hadharani kikosi chake kitakachocheza na Alikiba
Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam mnamo Juni 9, 2018 .
_______________________________________________________________________________________________
Kwa sasa unaweza kupata habari zetu zote sehemu moja kwa kupitia App yetu ya Bongo5. Pakua sasa kupitia Play Store kwa kubonyeza link hii – https://bit.ly/2J2Argw