BASATA watoa neno kufuatia taarifa za Ommy Dimpoz kurejeshwa Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu
Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) limetoa neno kwa mara ya kwanza tangu siku ya jana taarifa zisambae mitandaoni kuwa msanii wa muziki nchini Tanzania, Ommy Dimpoz amerejeshwa Afrika Kusini alikokuwa akipatiwa matibabu.
Taarifa ya BASATA hiyo ya BASATA imetoka yakiwa yamepita masaa 24 tangu kuenee kwa taarifa hiyo ya kuumwa tena kwa Ommy Dimpoz.
Imeripotiwa tena msanii na ndugu yetu @ommydimpoz amerejea hospitalini kwa matibabu zaidi. Tunasimama na wapenda sanaa, wapenzi wake na watanzania wote kwa ujumla katika kumwombea na hatimaye arejee katika afya yake. Tusimame naye katika dua na kumtakia kila kheri katika matibabu yake. #getwellsoon#ommydimpoz from #basata
Ommy Dimpoz tangu mwezi Mei amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya Koromeo ambayo yalipelekea afanyiwe upasuaji nchini Afrika Kusini ambako hadi leo bado anaendelea na matibabu.
Mungu yupo pamoja nae
Ugua pole bro
Mungu awe nawe dimpoz
Basata nao kichwa maji jamani
Sasa uongozi wa rockstar ushatoa tamko kuwa hali yake ipo vizuri alienda kwa chek up tuu basi kwa muujibu wa madaktar kila baada ya miezi mitatu alipoti
Sasa nyie baraza eti mnatamka habari zinazoenea mtandaoni bila hata ya kuchunguza ivi baraza mpo serious kweli Jamani
Nimeamini baraza wao wanakagua vya mtandaoni ndio mana kesi nyingi za baraza zinahusu wasanii kukaa uchi mitandaoni
Mana hamuumizi bongo zenu kazk kufungia nyimbo tuu
Basata nao wanahusika Hapo !?
Wasije kumfungia asisafirishwe
Basata nao wanapenda kiki kama gigy 😂😂
Pole Kwake..
Shkamo basata
Kwani anaumwa nini