Burudani
Beyonce kuwa muimbaji Mmarekani Mweusi anayelipwa fedha nyingi kuwahi kutokea, ataingiza $200ml kwenye ziara yake
![](https://bongo5.com/wp-content/uploads/2013/04/tumblr_mlbh85SVb01rqgjz2o1_12801.jpg)
Beyonce anatarajiwa kuwa muimbaji wa Marekani mwenye asili ya Afrika anayelipwa fedha nyingi zaidi kuwahi kutokea, “Highest Paid Black Musician of All Time.”
Kwa mujibu wa MTV, Beyonce anatarajia kuingiza zaidi ya dola milioni 200 baada ya kumalizika kwa ziara yake ya ‘Mrs Carter Show World Tour’ mwaka huu. Ziara hiyo ambayo tayari ni ziara ya msanii wa kike iliyoingiza fedha nyingi zaidi mwaka 2013, mwaka huu inatarajiwa kuwa ya mafanikio zaidi katika maisha yake ya muziki na kumfanya ‘the highest paid black musician of all time!”
Hiyo ina maana kuwa Beyonce atawazidi Mariah Carey, Diana Ross na Janet Jackson.