Habari

Dar Mpya ya Makonda: Makonda afanya ziara jijini Dar kusikiliza kero za wananchi

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda ameanza ziara yake ya siku 10 ndani ya jiji la Dar es salaam kwa ajili ya kusikiliza kero za wananchi pamoja na kuzitafutia ufumbuzi.
4k0a3112
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akitoa maagizo kwa baadhi ya viongozi

Ziara hiyo imeanzia katika wilaya ya Kigamboni ambapo kabla ya kwenda kusikiliza kero za wananchi mtaani, Mkuu huyo alizungumza na viongozi wa wilaya hiyo pamoja na kuzindua mpango mkakati wa Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa.

Akiongea na viongozi hao wa wilaya ya Kigamboni, Makonda amesema anafanya ziara hiyo ili kugundua kero za wanachi pamoja kuwahamasisha wafanyakazi wa serikali kuwajibika.

“Nataka wafanyakazi wafanyekazi kwa bidii ili kuendana na kasi ya Rais wetu, nimegundua 80% ya wafanyakazi wa serikali hawafanyikazi, asilimia 80 ya watumishi wa umma hawafanyikazi, niwapiga majungu, wasoma magazeti, niwambea. Kilichobaki ni kusubiri mwisho wa mwezi kwa ajili ya mshahara,” alisema Mkonda.

Pia Makonda alisema hataki kuona wananchi wanakimbilia kwa mkuu wa mkoa kuomba msaada wa utatuzi wa changamoto zao wakati serikali ina wafanyakazi kuanzia ngazi ya vitongoji.

Aidha mkuu huyo ataelekea mtaa wa Maweni, Mjimwema ambapo ataangalia uharibifu wa mazingira uliosababishwa na wachimba kokoto.

4k0a3123

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni,Hashim Mgandilwa akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Kinondoni Paul Makonda

4k0a3154

Viongozi na watumishi wa idara mbalimbali za Wilaya ya  Kigamboni

4k0a3155

Mkuu wa Wilaya na Kinondoni Ally Hapi

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents