Burudani

Diamond ni mwanamziki wa kipaji halisi – Yericko Nyerere

Mwanachama wa Chadema Yeriko Nyerere amesema kuwa yeye kuwa amemsikiliza AliKiba na Diamond na kusema kuwa Diamond ni mwanamziki wa kipaji halisi.

Kada huyo wa Chadema ametweet maneno hayo kupitia ukurasa wake wa Tweeter leo kuonyesha hisia juu ya wasanii hao ambao wote wametoa nyimbo kwa kufuatana.

“Si shabiki wa miziki ya wabana pua wanaooga mara sita kwa siku, lakini nimesikiliza Kiba na Diamond, Diamond ni mwanamziki wa kipaji halisi.” ameandika Yericko Nyerere.


Hata hivyo baada ya post hiyo mashabiki wa pande zote mbili walishusha comment mbalimbali ambapo Yericko Nyerere amesema katika hizo nyimbo ya Diamond ni nzuri.

Mpaka sasa wimbo mpya wa Alikiba ‘Seduce Me’ ulioachiwa Ijumaa hii unaendelea kutrend kupitia mtandao wa video wa YouTube huku nafasi ya pili ukifuatiwa na wimbo mpya wa WCB, Zilipendwa.

Na Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents