Burudani
Exclusive: Fid Q kutoa ‘mini documentary’ ya ‘Siri ya Mchezo’ ambamo maprofesa watafanya uchambuzi
Rapper Fareed Kubanda aka Fid Q amesema mashabiki wasitarajie kuona video ya wimbo wake mpya, ‘Siri ya Mchezo’ aliomshirikisha Juma Nature. Badala yake, atatoa mini documentary ya wimbo huo.
“Hatutoi video ya Siri ya Mchezo, isipokuwa tunatoa mini documentary ambamo ndani tunatarajia kuwa na maprofesa, dakika 15, watachambua wao,”Fid aliiambia Bongo5.
Alisema kazi ya utengenezaji wa documentary hiyo itamalizika ndani ya wiki mbili zijazo.
Fid aliongeza kuwa ameamua kutoa mini documentary na si video ya Siri ya Mchezo ili watu waweze kuelewa zaidi dhana ya Kitaaolojia ambalo ni jina la albam yake ijayo. Msikilize hapo chini.