Burudani
Feza Kessy na washiriki wengine wa zamani 9 warejea Big Brother!
Shindano la Big Brother Africa limechukua sura mpya baada ya washiriki wa zamani wa shindano hilo kuingia mjengoni na kuwa housemates wa Hotshots.
Hatua hiyo iliwashangaza housemates wa sasa huku mashabiki wakidai kuwa Big hajawatendea haki hasa kwakuwa nao pia watawania fedha hizo.
Housemates are shocked when Biggie announces that 10 former #BigBroAfrica housemates will be competing with them. #BBHotshots
— Big Brother Africa (@BigBroAfrica) November 16, 2014
Washiriki hao wa zamani waliorejea kwenye mjengo huo ni pamoja na Feza Kessy, Miss P wa Botswana, Miss_Vimbai wa Malawi, Luclay wa Afrika Kusini, Uti wa Nigeria, Elikem wa Ghana, Sulu wa Zambia, Leone wa Zimbabwe na Uganda ni Denzel.