Habari
Future adai alimchumbia Ciara sababu muda wa kuoa umewadia
![](https://bongo5.com/wp-content/uploads/2013/11/future-ciara.jpg)
Rapper wa Atlanta, Future anasema yupo tayari kumuoa Ciara kwasababu amefikia umri katika maisha ambao anatakiwa kutulia.
“Umri unaenda,”alisema rapper huyo mwenye miaka 29, aliyemvisha pete ya uchumna Ciara mwezi uliopita. “Una maisha ya mara moja ya kuishi. Hivyo nayaashi kwa namna ninayotaka kuyaishi.”
Future alisema yeye na Ciara bado hawajapanga tarehe ya kufunga ndoa lakini wanazo kadhaa kichwani. “Tunataka tarehe iwe special. Tunajaribu kuchagua tarehe.”
Baada ya kuwa wapenzi kwa mwaka mmoja, Future alimchumbia Ciara kwa pete yenye thamani ya takriban shilingi bilioni 1 kwenye birthday yake Ciara New York.