Habari
Hisa moja ya Twitter yauzwa kwa zaidi ya shilingi 73,000
Hisa za mtandao wa Twitter jana zimeuzwa kwa $44.90 (zaidi ya shilingi 73,000) ikiwa ni asilimia 73% zaidi kutoka kwenye bei yake ya kwanza ya $26 kila moja.
Waasisi wa Twitter Jack Dorsey, Evan Williams na Biz Stone wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya hisa za Twitter kuingia (IPO) jana
Hiyo ina maana kuwa baada ya siku ya kwanza ya kampuni hiyo kuwa ya umma, Twitter sasa inathamanishwa kwa dola bilioni 31.
Zaidi ya hisa milioni 13 ziliuzwa saa moja tu baada ya kuingia sokoni kufutia soko la hisa la New York kufunguliwa.
Twitter ina watumiaji milioni 230 lakini bado haijaanza kupata faida.