Burudani
Izzo Bizness adai hawezi kutoa wimbo bila mama yake kuupitisha
Rapper Emmanuel Simwinga aka Izzo Bizness, amesema kabla hajatoa wimbo ni lazima ampe mama yake ausikilize kwanza.
Izzo ameliambia gazeti la Mtanzania kuwa tabia hiyo aliianza baada ya kutoa wimbo wake wa kwanza wa ‘Bizness’ na alipoupitisha ukawa na mafanikio makubwa.
“Huwa namtumia nyimbo mbili kisha yeye anachagua upi niutoe,” alisema.
“Nipo tofauti na wasanii wengi ambao kabla hawajatoa wimbo huwa wanawapa watangazaji, madj na wadau wengine wa muziki. Lakini mimi mama yangu ndio amekuwa mchaguzi wa nyimbo zangu.”