Habari
Janet Jackson na Wissam Al Mana walifunga ndoa kwa siri mwaka jana
Janet Jackson na mume wake Wissam Al Mana wamethibitisha kwenye maelezo kuwa tayari wamefunga ndoa tangu mwaka jana.
Hii ni ndoa nyingine ya siri ya Janet ambapo maelezo yao yalisomeka.
“Tetesi kuhusiana na harusi ya kifahari si kweli. Mwaka jana tulifunga ndoa kwenye sherehe tulivu, private na nzuri. Zawadi zetu za harusi kwetu sisi wenyewe zilikuwa ni kuchangia vituo vya watoto wasio na uwezo tuvipendavyo.Tungefurahi kuwa maisha yetu binafsi yanaheshimiwa na kwamba tunahuruhusiwa kuwa na muda huu wa kusherehekea na furaha. With love, Wissam and Janet”