Burudani
Jay-Z na Rihanna kutumbuiza kwenye sherehe za ufungaji wa Paralympics
Jay-Z , Rihanna na kundi la Coldplay watatumbuiza kwenye sherehe za kufunga mashindano ya Olimpiki kwa watu wenye ulemavu Jumapili ijayo (09.09.12) jijini London Uingereza.
Gazeti la Daily Mirror limesema kuwa kiongozi wa Coldplay Chris Martin ndiye aliyemshawishi Jay-Z kushiriki.
Vyanzo vimesema show hiyo inategemea kuhudhuriwa na mashabiki wengi wa wanamuziki hao na kwamba sherehe hizo za ufungaji wa Paralympics zitafana kuliko miaka ya nyuma.
Mashindano ya Paralympics huanza muda mfupi baada ya kumalizika kwa Olimpiki ya kawaida.