Burudani
Jux: Vee Money mshkaji wangu tu
Muimbaji wa ‘Uzuri Wako’ Jux amekanusha tetesi za mtaani kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na hitmaker wa ‘Come Over’ Vanessa Mdee aka Vee Money.
Jux aliyekuwa akihojiwa kwenye ‘You Heard’ ya XXL, Clouds FM leo kwa simu nchini China wakato akiwa location akishoot video ya wimbo wake mpya ‘Nitasubiri’, Jux alidai kuwa Vanessa ni rafiki yake tu na hakuna uhusiano mwingine zaidi ya huo.
“Hamna mshkaji wangu, rafiki yangu tu hakuna kitu chochote kinachoendelea,” alisema Jux kukanusha tetesi hizo.