Habari
Kaka wa rapper Trina auawa kwa risasi
Wilbrent Bain, aliyetambuliwa na polisi kama kaka wa rapper Trina, ameuawa jana baada ya kupigwa na risasi huko Miami nchini Marekani.
Polisi wamedai kuwa Bain alikuwa akiendesha baiskeli na ndipo kijana mwenye miaka 27, Ron Dobson alipochukua bunduki na kuanza kumshambulia kwa risasi. Polisi wamesema Bain hakuwa na silaha ambapo wawili hao walikuwa na beef la muda mrefu.
Dobson alikamatwa na kukiri kuhusika na mauaji hayo. Mpaka sasa Trina hajasema chochote.