Burudani
Khloe Kardashian alimpiga chini French Montana baada ya kugundua anammendea rafiki yake
Khloe Kardashian anadaiwa kuwa aliamua kumpiga chini mpenzi wake French Montana mapema mwezi huu baada ya kugundua kuwa alikuwa akimmendea rafiki yake..
Khloe na Malika
Kwa mujibu wa mtandao wa Media Take Out, Khloe aligundua kuwa mpenzi wake alikuwa akitumiana ujumbe wa simu kwa siri na rafiki yake Malika Haqq.
French Montana na Malika (kulia)
Chanzo kimoja kiliuambia mtandao huo kuwa Khloe alizigundua sms hizo aliposhika simu yake. Hata hivyo kimesema kuwa urafiki wa Khloe na Malika bado upo palepale na kwamba hakuwa akimpenda Montana kwa dhati.