Michezo
Beki wa Liverpool kuwa nje msimu mzima baada ya kuumia
Klabu ya Liverpool imepata pigo baada beki wake kushoto Joe Gomez kuumia na atakua atakuwa nje ya uwanja kwa msimu uliobaki. Gomez mwenye umri wa 18 aliumia goti wakati akiichezea timu ya taifa ya England chini ya miaka 21 katika mchezo dhidi ya Kazakhstan.
Kinda huyo amecheza michezo mitano ya ligi kuu msimu huu toka alipojiunga na Liverpool akitokea timu ya Charlton kwa dau la pauni million 3.5.
Kocha mpya wa Liverpool Jurgen Klopp anatarajia kuanza mchezo wake wa kwanza siku ya Jumamosi dhidi ya Tottenham huku akikosa huduma ya beki huyo.