Habari
Lema awasili Polisi kuitikia wito
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Godbless Lema amewasili kwenye Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha SACP Ramadhan Ng’anzi kuitikia wito uliomtaka kufika kwenye ofisi hizo kwaajili ya mahojiano.
Kwamujibu wa chombo cha habari cha Azam, Mbunge huyo aliyekuwa ameambatana na Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Arusha Elisa Mungure amefika ofisini hapo majira ya saa 4:55.
Hata hivyo bado haijafahamika rasmi kusudio la kuhitajika kwake polisi juu ya mbunge huyo.