Burudani
Linah akiri kuwa mtandao wa Instagram umekuwa ukimliza na kumsononesha mara nyingi
Muimbaji wa ‘Ole Themba’ Linah amekiri kuwa mara nyingi mno amekuwa akilia kutokana na comments za Instagram.
Ameiambia Bongo5 kuwa kinachomuuma zaidi ni watu kumdharau kuwa ni mfupi ilhali wakijua kuwa ndivyo alivyoumbwa.
“Ofcourse nakubali kwamba mimi ni mfupi, it’s fine, ndivyo nilivyoumbwa lakini so far nipo short but sexy wazungu wanasema, kwahiyo najiamini,” amesema mrembo huyo.
“Instagram imewahi kuniliza kwasababu najiuliza mbona imekuwa too much, kwanini imekuwa hivyo. Kwahiyo lazima nilie. Nikiomba ushauri naambiwa ‘Linah mti wenye matunda matamu haushi kupigwa mawe kwahiyo shukuru Mungu kuna baadhi wanatamani hata hivyo hawapati kwahiyo inamaanisha watu wanakufuatilia’.
Msikilize zaidi hapo chini.