Habari

Maafisa wa Nigeria wakamata gunia 102 za ‘mchele wa plastiki’

Sakata la ‘mchele wa plastiki’ bado linaendelea kushika kasi katika nchi mbalimbali za Afrika baada ya Tanzania hivi karibuni kukanusha kuwepo kwa mchele huo. Huko nchini Nigeria maafisa wa nchi hiyo wamekamata magunia 102 ya ‘mchele wa plastiki’ yaliyokuwa yanaingizwa nchini humo na wafanyabiashara haramu ambao walitaka kuuza katika msimu huu wa sherehe, kulingana na afisa wa forodha katika mji mkuu wa nchi hiyo , Lagos.

Uchunguzi wa awali ulibaini kuwa mchele huo ulikuwa ni wa “plastiki” ,baada ya kuuchemshwa, na kuoneka kuwa mkubwa zaidi ya mchele wa kawaida na ni Mungu tu anajua ni nini ambacho kingetokea kama ungeliwa na binadamu “, Haruna Mamudu aliongeza katika kauli yake juu ya tukio hilo.

Aliwawaonya wahujumu wa uchumi ambao wanangalia kipindi hiki cha sherehe kama njia za kupata mapato kwa udanganyifu kuwa watakabiliwa na mkono wa sheria.

Bwana Mamudu hakuelezea ni vipi mchele huo wa plastiki ulitengenezwa lakini ulikua na nembo iliyoandikwa “Best Tomato Rice”.

Uchunguzi unaendelea kutambua ni kiwango gani cha mchele huo kimekuwa kikiuzwa na ni vipi unaweza kuondolewa sokoni ili kulinda afya za raia wa Nigeria waliokwisha utumia na kuwapeleka wahusika wa biashara hiyo haramu mbele ya sheria”.

Nchini Uchina, kuliwahi kuwa na sakata ya chakula mwaka jana baada ya kubainika kuwa kuwepo kwa mchele uliotengenezwa kwa plastic.

Nchini Tanzania Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), iliwatoa hofu Watanzania kuhusu taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa kuna mchele unaotengenezwa kwa plastiki kutoka nchini China.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents