Burudani
Makamua, Fid Q, Saigon, One, Songa na Lamar kuonekana kwenye filamu kuhusu dawa za kulevya
Makamua, Fid Q, Saigon, One, Songa na Lamar wataonekana kwenye filamu inayozungumzoa matumizi na athari za dawa za kulevya
Makamua amekiambia kipindi cha Planet Bongo cha EATV kuwa Fid Q, Saigon, One, Songa na Lamar watavaa uhusika na kuonyesha uhalisia wa matukio.
“Mimi nimeigiza kama Joseph pia wahusika wengine ni One the Incredible, Peter Msechu, Lamar, Songa na Saigon na wengine wengine,” amesema Makamua.
“Movie inahusika na kwenda agaist na drug abuse, kwahiyo watu wa East Africa, watu wa Afrika ya kati wakae tayari kwa kupata kitu ambacho kipo kwenye uhalisia kabisa. Kwa sababu tunaishi katika mazingira ambayo watu hawataki kuonyesha maisha yao katika upande mwingine. Mashabiki wanataka kujua.”