Michezo
Man City wakamilisha usajili wa Leroy Sane kutoka Schalke 04
Klabu ya Man City ya England leo August 2 2016 imetangaza rasmi kukamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji ambaye pia ana uwezo wa kucheza nafasi ya winga Leroy Sane kutoka Schalke 04.
Huu unakuwa ni usajili wa pili wa Man City wakiwa na kocha wao Pep Gurdiola baada ya usajili wa kwanza wa Gundogan, wamethibitisha kumsajili Leroy Sane kutoka Schalke 04 kwa ada ya uhamisho wa pound milioni 37 na kumpa mkataba wa miaka mitano staa huyo.