Michezo
Maria Sharapova anyakua taji la Porsche Grand Prix kwa kumshinda Ana Ivanovic
Mchezaji namba sita kwa ubora duniani katika tennis upande wa wanawake, Maria Sharapova amemshinda Ana Ivanovic na kunyakua taji la Porsche Tennis Grand Prix kwa mara ya tatu huko Stuttgart.
Mrusi huyo, 27, alishinda kwa 3-6 6-4 6-1 na kushinda taji lake la 30.
Katika hatua nyingine mchezaji namba mbili wa tennis duniani kwa wanaume, Novak Djokovic ametangaza kuwa yeye na mchumba wake Jelena Ristic wanatarajia kupata mtoto. ‘Jelena is pregnant!!! We will be parents soon! #blessed’
Jelena Ristic
Wawili hao wamekuwa pamoja kwa takriban miaka tisa.