Burudani
Mkasa mzima uliomtokea Mlinzi wa Drake
Mlinzi (Security Guard) wa nyumba ya msanii Drake amejeruhiwa na kukimbizwa Hospitali baada ya shambulio la risasi lililoripotiwa kutokea nje ya Nyumba ya Rapa huyo mapema leo mjini Toronto Canada.
Polisi wa Toronto walifanya uchunguzi juu ya tukio hilo ambalo limebainika kweli majeruhi huyo ni Mlinzi wa Drake inadaiwa wakati wa tukio hilo linatokea Drake hakuwepo nyumbani.