Mourinho awasili Ureno kwa mazishi ya baba yake mzazi (+Picha)
Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho tayari ameshafika nchini Ureno kwa ajili ya mazishi ya baba yake mzazi.
Baba yake Mourinho aitwae Jose Manuel Mourinho Felix 79 amefariki Dunia wikiendi iliyopita baada ya kuugua kwa muda mrefu na mazishi yanatarajiwa kufanyika leo huko jijini Setubal nchini Ureno.
Mapema jana Mourinho kupitia ukurasa wake wa Instagram aliweka picha ya baba yake huku ikiwa na rangi nyeusi na nyeupe (B&W) na hakuandika kitu huku maoni ya mashabiki wakionekana kumpa pole kwa msiba uliompata.
https://www.instagram.com/p/BVxoRvQAZT2/?taken-by=josemourinho
Katika enzi za uhai wake Baba mzazi wa Mourinho alishawahi kuitumikia timu ya taifa ya Ureno na Klabu ya Victoria Setubal FC kwa michezo 250.
Tazama picha za Mourinho alivyowasili Ureno kwa kwa ajili ya mazishi ya baba yake mzazi.