Burudani
Mr Blue achimba mkwara, ‘watoto wameshacheza sana muda wao wa kwenda kulala umefika’
Mr Blue ametangaza kuwa anatarajia kuvunja ukimya kwa kuachia kazi mpya.
Kupitia Instagram, Blue ameandika:
Nawashukuru sana wadau wangu wa kazi zangu…kazi inakuja kazi mpya kutoka kwa kijana wenu imefika takribani miaka mitatu sasa toka nilipotoa nyimbo yangu ya mwisho :”PESA”:. ambayo mpaka leo bado ipo namshukuru muumba aliyenipa kipaji cha kutengeneza nyimbo zinazodumu ..watoto wameshacheza sana mda wao wa kwenda kulala umefika nafikiri wote mnajua kuwa watoto wanatakiwa kulala mapema hasa baba anapokuwa amerudi…nawapenda mashabiki zangu na napenda mnavyonivumilia…#onelov#