Msanii Alikiba amewapa ujumbe huu mashabiki wake ikiwa leo ni siku yake ya kuzaliwa
Shukrani zangu kwa mashabiki mwaka huu katika #FungaMwakaNaKingKiba zinakuja na show mbili kubwa ndani ya December 2018."
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Ali Salehe Kiba alimaarufu Alikiba, amefunguka mengi kwenye ukurasa wake wa Instagram ikiwa ni siku yake ya kuzaliwa.
Msanii huyo ameweza kutoa shukrani kwa mashabiki zake na kusema ;- ” Ikiwa leo ni siku yangu ya kuzaliwa namshukuru Mungu kwa kuendelea kunibariki katika kila jambo na namshukuru kwa kunipa mashabiki wanaonipa support ya dhati kabisa. Shukrani zangu kwa mashabiki mwaka huu katika #FungaMwakaNaKingKiba zinakuja na show mbili kubwa ndani ya December 2018, 1st Edition ya Funga Mwaka Na King Kiba nitakuwa na Princess of Africa Mama Yvonne_ ChakaChaka itafanyika Serena Hotel Dar es salaam 22 .December. 2018
2nd Edition ya Funga Mwaka Na KingKiba itatukutanisha pale Next Door Arena, Dar es Salaam tarehe 29. December.2018.
Mark the dates and stay tuned for more information. Powered by Mofaya Energy Drink.
#MofayabyAlikiba
#King’sBirthday2018
#FungaMwakaNaKingKiba
#KingKiba”
By Ally Juma.