Burudani
Msanii Femi One wa Kenya aliyeimba ‘Utawezana’ sasa ni mama kijacho
Habari mpya mjini ni kuhusu ujauzito wa msanii maarufu wa nchini Kenya Femi One ambae amefahamika Africa nzima kupitia kibao ambao alimshirikisha Mejja kwa jina “Utawezana”.
Femi One ameonekana kufurahia hadi kufunguka kupitia mtandao wa instagram akionyesha jinsi ujaizito wake ulivyokua.
Mama kijacho huyo hatahivyo, ametaniwa na boss wake King Kaka kwa kutupia post inayoonyesha video fupi ya Femi One akiringia mashabiki wake ujauzito huo. King Kaka aliandika maneno haya ” Nikama kuna mtu amewezana” hata hivyo kunatetesi kua msanii Nviiri the story tellee kutoka kundi la Soul generation huenda akawa ndie mwenye ujauzito huo.
Imeandikwa na muandishi Changez Ndzai – Kenya