Burudani

Mshindi wa BSS 2015 Kayumba Juma ashusha mjengo huu Chamazi

Meneja wa mshindi wa BSS 2015 Kayumba Juma, Mkubwa Fella ameonyesha nyumba ya mshindi huyo wa BSS ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Kipepeo’.

IMG_0655
Nyumba ya Kayumba iliyopo Mbande Msewe Chamazi jijini Dar es salaam

Akiongea na Bongo5 Ijumaa hii, Fella alisema ameamua kuonyesha nyumba hiyo ili kuwajibu watu ambao wanapenda kujua matumizi ya pesa ambazo alishinda muimbaji huyo.

“Kayumba tayari ana nyumba hii hapa, sidhani kama tungeamua kuweka pesa mpaka sasa hivi zigekuwepo, lakini nyumba hii hapa, muda wowote akitaka anaamia,” alisema Fella.

Fella amesema wasanii wake wengi anawajengea nyumba kwa kuwa wasanii wengi wameshindwa kujiwekea kidogo wanachopata mpaka kufikia kiwango cha kujenga nyumba.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents