Habari

Mtangazaji wa BBC, Komla Dumor afariki dunia

Mtangazaji wa BBC TV, Komla Dumor amefariki dunia ghafla jana akiwa nyumbani kwake mjini London, Uingereza.Alikuwa na umri wa miaka 41.

Komla-Dumor

Dumor aliyezaliwa nchini Ghana alikuwa mtangazaji wa BBC World News na aliendesha kipindi cha Focus on Africa.

Mtangazaji huyo alijiunga na BBC kama mtangazaji wa radio mwaka 2007 baada ya kufanya kazi ya uandishi wa habari kwa zaidi ya muongo mmoja nchini Ghana. Rais wa Ghana, John Dramani Mahama aliandika kwenye mtandao wa Twitter kuwa nchi yake imepoteza mmoja wa mabalozi wake muhimu.

Inadai kuwa alifariki kwa mshtuko wa moyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents