Kufuatia Bondia Hassan Mwakinyo kufanya yake usiku wa kuamkia leo kule Visiwani Zanzibar baada ya kishinda kwa KO raundi ya 7 kwa kumdondosha mpinzani wake Mghana hatimaye amewasili Jijini Dar es salaam huku akipokelewa na mashabiki pamoja na wananchi Kifalme.
Mwakinyo alifanikiwa kuipeperusha Bendera ya Tanzania usiku wa kuamkia leo kwa kufanikiwa kubeba Mkanda wa WBO.